![azlyrics.biz](https://azlyrics.biz/assets/logo.png)
maralee dawn - rebekah lyrics
wakati mwingine nikiketi kukuimbia mie
huwa nalemewa kupata maneno yanayoshimiri
ni kama mtoto mchanga anapojaribu kueleza ukubwa wa sayari
ni kama kidege kinapojaribu kueleza upana wa mbingu
ni kama changarawe kujaribu kueleza ukubwa wa bahari
ukweli ni kwamba maneno yangu hayatoshi, hayawezi kueleza
hivyo daima na milele siku zote za maisha yangu
nitatafuta kukuimbia maneno yanayokufaa
wakati mwingine nikiketi kukuimbia mie
huwa nalemewa kupata maneno yanayoshimiri
ni kama tone la maji kujaribu kueleza mfuriko wa mvua
ni kama wapendanao kujaribu kueleza fumbo la penzi
ni kama mshumaa kujaribu kueleza kung’aa kwa jua
ukweli ni kwamba maneno yangu hayatoshi, hayawezi kueleza
hivyo daima na milele siku zote za maisha yangu
nitatafuta kukuimbia
maneno yanayokufaa
ni kama jiwe linapojaribu kueleza urefu wa mlima
ni kama sheha shupavu kujaribu kueleza hadithi zote za jadi
ni kama mwenye dhambi kujaribu kueleza neema ya msamaha
ukweli ni kwamba maneno yangu hayatoshi, hayawezi kueleza
hivyo daima na milele siku zote za maisha yangu
nitatafuta kukuimbia, nitatafuta kukuimbia
maneno yanaykuofaa
Random Lyrics
- wayne newton - nobody knows the trouble i've seen lyrics
- skia - apricot lyrics
- 6ix6ix6ix - подскажи (tell me) lyrics
- use soap. - me against mr. max martin lyrics
- cardinal black - tell me how it feels lyrics
- 23 (swe) - stationen freestyle lyrics
- springlike - listen lyrics
- blue gillespie - beat oven lyrics
- marion raw - run with the sea lyrics
- carl smith - pins and needles lyrics