azlyrics.biz
a b c d e f g h i j k l m n o p q r s t u v w x y z 0 1 2 3 4 5 6 7 8 9 #

p mawenge – my future wife lyrics

Loading...

[intro]
dear future wife, chuganian girl

[verse 1]
hivi nini baby w+ngu kilichofanya unidharirishe
mpaka majirani wananitukana ili niaibike
sema kama mimi ndo nlikukana usifiche
ka so wenyewe kuna bwana alikufanya ukipe
ulipotoka kwenu ni mimi ndo ulifwata
ingawa mabwana zako mjini walishajipata
ila sababu tu kijijini walikukacha
ukaona bora tu utulie na mimi tuanze chapta
nikakupa mahaba na ukadata nayo sana
nikajua lile penzi tungezikwa nalo mama
wala sikufikiri kuna siku tungeachana
na ungetumwa na mabwana zako uje kuntukana
kwanza hatukugombana hakuna nlichokufanya
ila ukatoka kw+ngu ukanza kuishi kwa kuhamahama
mi naletewa umbea tu unavochange mabwana

roho iliniuma haki nilisikitika sana
ukazungusha mwili kila kona ya mtaa
na hasa ulipagawa kila ulipoona mastaa
nilikonda watu wakajua nna ngoma kachaa
wakati mwanzo ulinikuta nimenona balaa
ukadanga sana ukijua utapata matajiri
ajabu wakakutosa kila ulipowapa mwili
dunia kijiji si ndo zikatapakaa siri

kwamba umewarudia wale walokutosa a city
hapo ndo nikajua kwamba huwapendi mahasla
unapenda mabishoo wenye vichenji vya ghafla
wanavyopata kwenye ki ki ki kitonga
hadi ukawapa ki ki ki kidonda
ulinishinikiza sana tuiandae future

tumwombe sana mola mana ndo atakayetupa
sa kwa nini boya alokutosa umvagae pupa
au ushamba baby umekufanya ukashangae supra
kisa machekibobu na wamеsokota virasta
yani wamekuchanganya kabisa mpaka umedata
ukisema “sina koloni” sa mbona umеlifuata
bila hata kujali walikuona kama takataka
najiuliza ni kipi cha siri wanachokupa
kusema kweli kwa hizi siku mbili umefutuka
umenona baby yani mpaka mwili umechanuka
ila punguza j+po kilo mbili mbili utapasuka
lakini kuwa makini, nenda kwa tahadhari
we ndo umedata nae ila mwenzio hana habari
na hata akiulizwa manzi gani anamkubali
anamtaja mwingine kwako we anapita tu safari

sasa leo cheki unanivua nguo hadharani
na tulishea nyumba hadi funguo za chumbani
kisa kakusitiri bwana ako huyo wa zamani
baby unabugishwa hivi ujinga huo ujinga gani
mara kibao nimejitahidi kukuskiza
kipindi wanaotujua wanapoamua kukuuliza
kisa mi na hao mabwana zako hatujawahi kuiva
ndo unanichukia mpaka unazuga hadi kujiliza

eti mabwana wa dar ujue wana dharau kweli
madem wa chuga wanatuona ka ma haugeli
wanamsifia uwoya tu anti ezekieli
wabaguzi sana siwataki tena wamefeli
sa mbona juzi kati hadi simu niliwapigia
j+po nlijua manzi w+ngu wananikanyagia
utofauti wetu pindi tunakufkuzia
sikupenda uwe kikwazo chetu kwenye hii dunia
dear future wife, jua kuwa umecheza rafu
wala sijafurahi wewe kunjazia watu
yote nilokufunza pindi ulipotua mjini
eti leo unatangaza we ndo wa kunishauri mimi
ndio najua kwenu ulishafunzwa na makungwi
lakini usibishe mi ndo nilikuongezea ufundi
ila chunga usije fanywa demu wa kundi
mana wewe bwana wako na mashem naskia mnashea uk+mbi
najua ni mashost hao ndo wamekuchochea
hata kuna vijembe ni wao walikuongezea
kipindi unanitusi walisimama kidedea
ila nikikinukisha wote gizani watatokomea

bwana ako si ndo yule mwana flani mwenye ugoko
ndo umedata kwake unampa penzi motomoto
mshaonekana sana pande nyingi za mitoko
na naskia umekubali mpaka k+mzalia mtoto
wale waoga tu, nawachukia for life
yani wameshindwa kwenye ngumi, wamehamia kwa wife
nawastahi tu ningeshawatia ma knife
hadi wakilala waniote nawajia ma night



Random Lyrics

HOT LYRICS

Loading...